Psalms 6:2-4


2 aUnirehemu Bwana,
kwa maana nimedhoofika;
Ee Bwana, uniponye,
kwa maana mifupa yangu
ina maumivu makali.

3 bNafsi yangu ina uchungu mwingi.
Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?


4 cGeuka Ee Bwana, unikomboe,
uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
Copyright information for SwhKC